Image: BBC

Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametangaza amri ya kutotoka nje ya wiki tatu kwa wilaya mbili zilizoathirika kuzuia maambuzi ya ugonjwa wa Ebola ya Sudani.

Amri hiyo ni sehemu ya masharti 21 ya kukabiliana na mlipuko mpya wa ugonjwa huo uliotangazwa nchini humo Septemba 20, 2022.

Mpaka kufikia jana watu 58 wamethibitishwa kuambukizwa Ebola, 19 wamefariki na 20 wamepona wakiwemo Madaktari na wafanyakazi wa sekta ya afya.

Katika hotuba yake kwa taifa usiku wa kuamkia leo masharti hayo aliyoweka ni pamoja na kuweka zuio kuanzia leo Jumapili la watu kutotoka nje katika wilaya za Mubende na Kasanda kuliko bainika mgonjwa wa kwanza.

Nyumba za Ibada zote zimefungwa pamoja na maeneo ya starehehe ikiwemo Baa, kumbi za disko, vibanda vya filamu pamoja na shughuli zote za michezo.

Usafiri wa umma na binafsi yaani mabasi, dalala, magari ya watu binafisi na boda boda kuuanzia leo zimezuiwa kutotembea usiku kuanzia saa moja jioni hadi saa kumi na mbili asubuhi.

Hatua hii ya Rais Museveni inafutiia ombi la chama cha Madaktari nchini humo mwezi jana kupitia kwa rais wao Samuel Oledo waliomba Rais Museveni kuziweka karantini wilaya zilizo na maambukizi.

Hata hivyo mpaka sasa wilaya tano ndizo zilizo na maambukizi lakini zikizoguswa ni mbili kunakotajwa ndiko chimbuko la mlipuko wa sasa.

View Comments