logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mhubiri na polisi watatu washtakiwa kwa madai ya ubakaji Uganda

Polisi wanasema muathiriwa alitapeliwa pesa zake na kunyang'anywa hati yake ya kusafiria.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri17 January 2023 - 12:48

Muhtasari


•Watatu hao walikamatwa kwa madai ya ubakaji wa mwanamke raia wa Latvia katika nyumba moja katika mji mkuu wa nchi hiyo, Kampala.

Mhubiri wa Uganda na maafisa watatu wa polisi wamekamatwa kwa madai ya ubakaji wa mwanamke raia wa Latvia katika nyumba moja katika mji mkuu wa nchi hiyo, Kampala.

Polisi wanasema muathiriwa alitapeliwa pesa zake na kunyang'anywa hati yake ya kusafiria.

Haijafahamika bado iwapo washukiwa wametoa maoni yao kuhusu mashtaka hayo.

Mhubiri huyo alikuwa amemwalika mwanamke huyo kuzuru nchini Uganda na aliwasili takriban mwezi mmoja uliopita, taarifa ya polisi ilisema.

Maafisa watatu walioshughulikia kesi hiyo wakati muathiriwa alipowasilisha malalamiko yake katika kituo cha polisi cha Jinja Road wanakabiliwa na mashtaka ya utovu wa nidhamu.

Muathiriwa anawashutumu kwa kumfungia mbaroni na kumlazimisha kuweka sahihi katika taarifa ya kukiri kupokea malipo ya pesa zake zote na kufutwa kwa kesi dhidi ya mhubiri.

Idara ya polisi ya Upelelezi wa Jinai sasa imechukua kesi hiyo na kumtaka yeyote aliye na malalamiko dhidi ya mhubiri huyo kuripoti kwao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved