logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanafunzi 4 wafariki, 20 wajeruhiwa baada la lori kugonga na kuangusha ukuta wa darasa

Shule hiyo ilifungwa ghafla hadi Jumatatu wiki kesho kwa mshangao kwa wanafunzi.

image
na Radio Jambo

Habari15 March 2023 - 09:38

Muhtasari


• Dereva alishindwa kulidhibiti lori kwa kona na kugonga lango la shule lakini lori halikusimama na likafululiza hadi kwa madarasa.

Lori aina ya Tipper lililogonga ukuta wa darasa.

Wanafunzi wanne wamethibitishwa kufariki dunia na wengine 20 kujeruhiwa baada ya lori kugonga chumba cha darasa katika Shule ya Sekondari ya Kasaka iliyoko Halmashauri ya Mji wa Kanoni, Wilaya ya Gomba, nchini Uganda.

Kulingana na picha ambazo zilichapishwa kwenye mitandao ya kijamii kutoka nchini humo, lori hilo aina ya tipper linaonekana limepiga dafrau ukuta wa shule hiyo na kuubomoa kabisa pamoja na kuathiri sehemu ya paa la darasa hilo.

Polisi walisema kwamba tukio hilo lilijiri mwendo wa saa nane na nusu alasiri ya Jumatano wakati wanafunzi walikuwa darasani kwa mahudhurio ya masomo.

Wanafunzi watatu wa kati ya gredi ya 2 hadi ya 5 walifariki kwa majeraha kiasi huku wan ne akifariki baada ya kukanyagwa kiasi cha kutoweza kutambulika.

Atatambulishwa baada ya uchunguzi wa DNA kufanyiwa mabaki yaliyokusanywa kutoka eneo hilo la tukio.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Kefasi Katumba aliiambia Monitor kuwa dereva wa lori la Sinotruk aligonga lango la shule kwanza kabla ya kugonga maabara ya kompyuta na darasa la Senior Four West.

“Dereva anaonekana alishindwa kulidhibiti gari kwa kona na akafikiri lori litasimama iwapo atagonga lango la shule. Kwa bahati mbaya, liliendelea tu kusonga mbele kwa kasi, likaanguka kwenye maabara ya kompyuta ambapo liliua wanafunzi wawili papo hapo na kujeruhi wengine kadhaa. Lori hilohilo lilisonga mbele na kugonga darasa la Senior Four West ambapo pia liliua angalau mwanafunzi mmoja papo hapo na kuwajeruhi wengine,” alisema.

Zaidi ya hayo, wasimamizi wa shule walilazimika Jumanne jioni kuwarudisha wanafunzi wengine nyumbani hadi Jumatatu ijayo huku wakipata nafuu kutokana na mshtuko kufuatia mkasa huo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved