In Summary

• Mlinzi huyo mtuhumiwa alichimba mitini na polisi walianzisha msako dhidi yake.

Mwanafunzi ajiua kwa kujipiga risasi Kilimanjaro
Image: YoutubeScreengrab

Mlinzi mmoja katika kampuni ya kibinafsi ya ulinzi mjini Kampala yuko mbioni baada ya kudaiwa kumpiga risasi mwenzake na kumuua katika nyumba yao ya kupanga eneo la Kalule, Parokia ya Lukuli, Tarafa ya Makindye, vyanzo kadhaa vya habari nchini humo vimeripoti.

 John Mujumbi, mlinzi mwenye umri wa miaka 25 anayehusishwa na Capital Guards and Patrol alidaiwa kupigwa risasi na mwenzake na mwenzake, Peter Ochoroi, 26, mwendo wa 12:30pm kufuatia kutoelewana siku ya Jumamosi kuhusu maegesho ya magari.

Wawili hao walikuwa katika kampuni moja ya ulinzi na wamekuwa wakishiriki chumba cha kukodi kilichotolewa na mwajiri wao.

"Walinzi wote wawili walikuwa na bunduki za SAR, kila moja ikiwa na risasi tano. Jukumu lao lilikuwa kutoa usalama katika vyumba vya IDAK huko Konge wakati wa usiku, kulingana na maagizo ya msimamizi wao,” naibu msemaji wa polisi, ASP Luke Owoyesigyire alinukuliwa na jarida hilo.

Walioshuhudia waliambia polisi kwamba walisikia mabishano kati ya walinzi hao wawili, yakiendeshwa kwa lugha wasiyoielewa na muda mfupi baadaye, mlio wa risasi ulisikika ukitokea katika chumba kimoja.

"Polisi walijibu haraka eneo la tukio, wakiandamana na timu ya tarafa na eneo la maafisa wa uhalifu. Mwathiriwa alikimbizwa mara moja katika Hospitali ya Mulago, ambako alitangazwa kufariki alipofika,” ASP Owoyesigyire aliongeza.

Tukio hilo linaripotiwa wiki moja baada ya tukio sawia la mlinzi kumshambulia bosi wake ambaye alikuwa waziri wa leba wan chi hiyo, Okello Engola.

View Comments