In Summary

•Bw Vormawor atazuiliwa na polisi kwa muda wa wiki mbili kisha afike mahakamani. 

Mahakama

Mwanaharakati wa Ghana aliyezuiliwa ambaye alikuwa mwandalizi mkuu wa maandamano ya hivi majuzi ya kupinga uchimbaji madini amenyimwa dhamana pamoja na wengine 11, licha ya kuwa mgonjwa mahututi.

Oliver Barker Vormawor alifikishwa mahakamani siku ya Alhamisi na kukana mashtaka mengi, yakiwemo kukusanyika kinyume cha sheria na kumshambulia afisa wa umma.

Bw Vormawor atazuiliwa na polisi kwa muda wa wiki mbili kisha afike mahakamani. Amekuwa akitibiwa katika hospitali ya polisi kwa ugonjwa ambao haukujulikana.

Mwanaharakati huyo ambaye ni mhitimu wa Cho kikuu cha Cambridge alipanga maandamano ya siku tatu kupinga hatua dhidi ya uchimbaji haramu wa madini, unaojulikana kwa kienyeji kama "galamsey", ambao umelaumiwa kwa kuchafua 60% ya maji ya Ghana.

View Comments