logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Si jukumu letu kuamua mawakili halisi wa IEBC - Mahakama ya upeo

Mwilu alisema makamishna hao wanne wanaweza kutumia huduma za Paul Muite

image
na Radio Jambo

Habari30 August 2022 - 14:01

Muhtasari


  • Mahakama ya upeo imesema si jukumu lake kusuluhisha ni wakili gani atakayewakilisha IEBC katika Mahakama ya Juu

Mahakama ya upeo imesema si jukumu lake kusuluhisha ni wakili gani atakayewakilisha IEBC katika Mahakama ya Juu.

Katika uamuzi wake Jumanne, Naibu Jaji Mkuu Philomena Mwilu alisema mzozo kati ya makamishna ni wa ndani.

"Mahakama hii haiwezi kushughulikia suala au mzozo wa uwakilishi wa kisheria wa IEBC katika ombi hili," alisema.

"Tumezingatia shauri. Sio shughuli ya mahakama bali ni suala la ndani ambalo lazima lisuluhishwe na IEBC na makamishna. Mahakama hii haitoweza. kuingizwa kwenye mzozo huu."

Mwilu alisema makamishna hao wanne wanaweza kutumia huduma za Paul Muite kama wataona ni muhimu katika shughuli hiyo.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved