In Summary
  • Juhudi za mamake mtoto huyo kuokoa mtoto wake kutokana na kipigo hicho hazikuzaa matunda kwani mwanamume huyo alimtishia
Image: CLAUSE MASIKA

Baba wa kambo ambaye aligeuka mkali na kumpiga mtoto wa miaka miwili kwa kujisaidia haja kubwa nyumbani kwake Ijumaa alishtakiwa katika mahakama ya Kibera.

Mahakama ilisikia kwamba TS alitumia mkanda na slippers kumpiga mtoto huyo mnamo Septemba 12 huko Kangemi ndani ya kaunti ya Nairobi.

Alikanusha mashtaka mbele ya hakimu mkuu wa Kibera Ann Mwangi na kuomba aachiliwe kwa dhamana.

Mahakama iliambiwa kwamba msichana huyo mdogo alijisaidia sakafuni bila hatia mbele ya mshtakiwa ambaye kwa kujibu alimpiga.

Juhudi za mamake mtoto huyo kuokoa mtoto wake kutokana na kipigo hicho hazikuzaa matunda kwani mwanamume huyo alimtishia.

Baadaye mtu huyo alikamatwa na siku ya Ijumaa alipandishwa kizimbani na kushtakiwa kwa kosa la kumpa mtoto adhabu ya kikatili kinyume na Sheria ya Mtoto.

Hakimu aliamuru mshtakiwa aachiliwe kwa bondi ya Sh100,000 au dhamana mbadala ya pesa taslimu Sh100,000 na mdhamini wa kiasi sawa na hicho.

Kesi hiyo itatajwa mapema mwezi ujao kwa ajili ya kusikizwa.

 

 

 

 

View Comments