logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tunapigwa, tunanyanyaswa na polisi - wakimbizi waiambia mahakama

Wawili hao waliitaka mahakama kuwaruhusu kurejea nchini mwao.

image
na

Habari23 May 2023 - 13:27

Muhtasari


  • Walikiri mashtaka na Ali Mustafa aliiambia mahakama kwamba alihitaji kwenda nyumbani ili aweze kuwahudumia watoto wake.

Wakimbizi wawili Jumanne waliambia mahakama ya Kibera kwamba walinyanyaswa na kupigwa na maafisa wa polisi wa Kenya walipokuwa kizuizini.

Wawili hao waliitaka mahakama kuwaruhusu kurejea nchini mwao.

Obura Hamza Okwri, Raia wa Uganda na Thiery Nishime, raia wa Burundi, walimweleza Hakimu Mkuu Mwandamizi wa Kibera Samson Temo kwamba hawakuwa tayari kuteseka zaidi mikononi mwa Mamlaka za Kenya.

"Polisi wamekuwa wakitupiga, tumeteseka hapa Kenya, turuhusu turudi katika nchi yetu," walisema kwa pamoja.

Wawili hao wanashtakiwa pamoja na Ali Mustafa na mkewe Sarah Abdullahi kwa kuanzisha fujo kwa namna ambayo huenda ikavuruga kuwepo kwa amani kinyume na sheria.

Hati ya mashtaka inasema washtakiwa walitenda kosa hilo mnamo Mei 22, 2023, saa 1200 katika Barabara ya General Mathenge katika Kaunti Ndogo ya Westlands ndani ya Kaunti ya Nairobi.

Mahakama ilisikia kwamba mshtakiwa alizua fujo kwa kuziba lango kuu la kuingilia na kurusha mawe moja kwa moja kwenye lango la afisi za Kituo cha Pamoja cha Huduma kwa Wakimbizi kilicho kando ya barabara hiyo.

Kulingana na mwendesha mashtaka wa mahakama Samson Ng’etich, washtakiwa ambao ni wakimbizi walitembelea maeneo hayo na kuanza kurusha mawe na kudai huduma fulani.

Walikiri mashtaka na Ali Mustafa aliiambia mahakama kwamba alihitaji kwenda nyumbani ili aweze kuwahudumia watoto wake.

Hakimu aliagiza washtakiwa wazuiliwe hadi Mei 30 kwa ajili ya ripoti ya uangalizi na ripoti ya watoto kuwasilishwa mahakamani.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved