logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mshukiwa wa mauaji ya Eric Maigo kuzuiliwa kwa Siku 21

Alihojiwa na DCI kabla ya kuzuiliwa katika kituo cha polisi cha Muthaiga.

image
na Radio Jambo

Habari27 September 2023 - 11:44

Muhtasari


  • Katika maombi tofauti, polisi wanasema kwamba mtoto huyo anaaminika ndiye alipanga vurugu zilizosababisha kifo cha Maigo mnamo Septemba 15.

Mshukiwa  anayedaiwa kumuua Mkurugenzi wa Fedha wa Hospitali ya Nairobi hospitalEric Maigo atasalia chini ya ulinzi wa polisi kwa siku 21 ili kuruhusu polisi kukamilisha uchunguzi.

Mtoto huyo mwenye umri wa miaka 16 alikamatwa siku ya Jumanne katika eneo la Kibra kaunti ya Nairobi.

Katika maombi tofauti, polisi wanasema kwamba mtoto huyo anaaminika ndiye alipanga vurugu zilizosababisha kifo cha Maigo mnamo Septemba 15.

Afisa huyo wa uchunguzi zaidi alisema kuwa mashahidi wakuu bado hawajarekodi taarifa na kuchukua sampuli za DNA kwa uchunguzi wa mkemia wa serikali.

"……afisa mpelelezi bado hajajua majeraha aliyopata wakati akitoroka kutoka eneo la uhalifu, kupeleka faili ya kesi kwa ODPP kwa ajili ya kuchunguzwa na kushauri na sio tu kuwasilishwa kwa walalamikiwa mbele ya mahakama kwa maelekezo zaidi," yasomeka maombi hayo mengine. .

Mtoto huyo, ambaye polisi walisema alikuwa anatoroka, alikamatwa katika kijiji cha Olimpiki huko Kibra, Jumanne usiku.

Alihojiwa na DCI kabla ya kuzuiliwa katika kituo cha polisi cha Muthaiga.

Maigo alipatikana akiwa na majerha 25 ya kuchomwa na visu kulingana na uchunguzi wa maiti.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved