logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Athari za kiafya zinazoambatana na kutumia sukari haramu

Shirika la KEBS waachalia sukari ghushi kuuziwa wakenya.

image
na Radio Jambo

Makala18 May 2023 - 06:43

Muhtasari


• Sukari hio iliyokamatwa na shirika hilo mwaka wa 2018 ilistahili kuharibiwa ama kurudishwa katika nchi ilyotoka kulingana na sheria.

• Shirika hilo lilibadilisha msimamo na kusema sukari hio inapaswa kubadilishwa kuwa ethanol ya viwandani.

Baadhi ya sukari iliyoharibika ambayo ilinaswa na maafisa wa DCI.

Jumatano, Rais William Ruto aliwapiga kalamu wahudumu wa serikali 27 baada ya kushukiwa kuhusika katika Sakata ya kuachilia sukari iiyokuwa imekamatwa na Shirika la Viwango la Kenya (KEBS).

Sukari hio iliyokamatwa na shirika hilo mwaka wa 2018 ilistahili kuharibiwa ama kurudishwa katika nchi iliyotoka kulingana na sheria.

Hata hivyo, shirika hilo lilibadilisha msimamo na kusema sukari hiyo ingebadlishwa kutumika kwa utengezaji wa kemikali aian ya ethanol. 

Licha ya mifuko hiyo ya sukari kuwekewa alama 'si salama kwa matumizi ya binadamu' wauzaji reja reja wanadaiwa kupakia upya sukari kwenye pakiti za kilo 1 na 2 za chapa ya sukari za humu chini miongoni mwao Kabras, Mumias Sugar na West Sugar na kuwauzia wakenya.

Lakini je, wafahamu athari za kutumia sukari hii?

Baadhi ya athari hizi ni:

Kama sukari hiyo ina chembechembe za zebaki (Mercury), sumu yake inaweza kuishia kuharibu mfumo wa fahamu wa mtu, kuwasababishia kupooza na kuhatarisha watoto ambao bado hawajazaliwa. Inaweza pia kusababisha Hyperactivity Disorder (Ugonjwa wa Upungufu wa Makini) kwa Watoto.

Pia kama sukari hio ina chembechembe za shaba inaweza kusababisha uharibifu wa ini, maumivu ya tumbo, kuhisi kichefuchefu, kuhara na kutapika.

Sukari hiyo ikiweza kuwa na Ukungu (Moulds) unaweza kuathirika na matatizo ya kupumua.

Sukari hio pia inashukiwa kuwa na chachu (yeast) hii inaweza kuathiri viungo vya ndani vya mwili.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved