logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sababu ya kufika mbele ya jopo la Azimio-Kalonzo Musyoka

Kalonzo sasa atasubiri jopo kuamua ni nani anafaa kuwa mgombea mwenza wa Raila.

image
na Radio Jambo

Makala10 May 2022 - 09:26

Muhtasari


  • Kalonzo sasa atasubiri jopo kuamua ni nani anafaa kuwa mgombea mwenza wa Raila

Kwa muda wa siku chache zilizopita kiongozi wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka amekuwa akijipiga kifua hangefika mbele ya jopo la Azimio.

Kulingana na Kalonzo mwaliko huo unadhalilisha na alikuwa akichagua mazungumzo na rais Uhuru kenyatta na mshirika wake Raila Odinga.

Hata hivyo akizungumza na wanahabari Kalonzo Musyoka, amefichua sababu iliyomfanya kuhudhuria mahojiano hayo huku akitoa maelezo ya kilichotokea ndani.

"Yalikuwa mazungumzo, si mahojiano. Niliamua kufika mbele ya jopo la Azimio kwa sababu hatukutaka kumpa mtu yeyote kisingizio cha kusema, 'aligomea kuja.' Yalikuwa mazungumzo ya ajabu.

Kalonzo sasa atasubiri jopo kuamua ni nani anafaa kuwa mgombea mwenza wa Raila.

Kalonzo alikuwa ameahidi kuondoka katika muungano huo iwapo wangemnyima nafasi ya naibu wa Raila akisema ndiye mgombeaji aliyefuzu zaidi hadi sasa.

“Kamati ina wanaume wakubwa na wazoefu kama Askofu Njenga na Askofu Zacheus Okoth, nililitazama hilo kivyangu na kusema kwa nini sitaki kwenda kukutana na Askofu Okoth? Ilibidi nifanye uamuzi huo.”


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved