logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Hatukuwasilisha karatasi zetu,'Irungu Kang'ata azungumza baada ya kunyimwa kibali na IEBC

Anasema hawakuwasilisha karatasi zao kwa vile muungano wa wawaniaji wao ulifungua kesi

image
na Radio Jambo

Yanayojiri06 June 2022 - 12:12

Muhtasari


  • Irungu Kang'ata azungumza baada ya kunyimwa kibali na IEBC
  • Anasema hawakuwasilisha karatasi zao kwa vile muungano wa wawaniaji wao ulifungua kesi ya kupinga uhakiki wao

Mwaniaji ugavana wa Murang'a Irungu kang'ata amefafanua kuhusu suala la uthibitishaji analodaiwa kuwa nalo na IEBC.

Kupitia kwenye ukurasa wake daktari wa falsafa katika sheria anasema kwamba hakuwasilisha karatasi zake kama inavyodaiwa kuripotiwa.

Anasema hawakuwasilisha karatasi zao kwa vile muungano wa wawaniaji wao ulifungua kesi ya kupinga uhakiki wao na hivyo walikuwa wakitafuta muda ili wachunguze pingamizi hilo kwanza kabla ya kuwasilisha karatasi zao kwa wakati ufaao.

"IEBC HAIKUkataa karatasi zetu au kukataa kutuidhinisha. Hatukuwasilisha karatasi zetu. Tulitafuta muda wa kusoma barua ya pingamizi iliyowasilishwa na muungano wa wagombea kupitia mwanasheria.Hatufungui shauri lolote.Tukishaisoma barua hiyo, tutawasilisha karatasi zetu." Aliandika Kang'ata.

Kang'ata ambaye anawania kwa tikiti ya UDA anatazamiwa kumenyana na Jamleck Kamau wa Jubilee na chama cha Wakulima Irungu Nyakera.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved