logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanawe Museveni Muhoozi afanya mazungumzo na Rais Uhuru

Baadaye, Muhoozi angedokeza kwamba ana nia ya kugombea Urais.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri08 June 2022 - 13:33

Muhtasari


  • Muhoozi, ambaye pia ni kamanda wa majeshi ya nchi kavu ya Uganda, alijadili masuala kadhaa ya pande mbili na ya kimataifa yenye maslahi kwa Kenya na Uganda

Jenerali Muhoozi Kainerugaba, mtoto wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni alimtembelea Rais Uhuru Kenyatta Jumatano katika Ikulu ya Nairobi.

Muhoozi, ambaye pia ni kamanda wa majeshi ya nchi kavu ya Uganda, alijadili masuala kadhaa ya pande mbili na ya kimataifa yenye maslahi kwa Kenya na Uganda.

"Miongoni mwa masuala yaliyojadiliwa ni pamoja na kurejesha amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo," Ikulu iliripoti.

Ziara ya Muhoozi nchini Kenya inajiri huku kukiwa na fununu kwamba anaweza kuwa analenga kumrithi babake Rais Museveni katika uchaguzi mkuu ujao wa nchi hiyo.

Mwezi Aprili, Jenerali huyo alizua tafrani nchini Uganda baada ya kufanya tafrija kubwa ya kutimiza miaka 48 ambayo ilihudhuriwa na babake Museveni na Rais wa Rwanda Paul Kagame.

Baadaye, Muhoozi angedokeza kwamba ana nia ya kugombea Urais.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved