logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Malkia Elizabeth II: Maisha katika picha

Elizabeth Alexandra Mary Windsor alizaliwa tarehe 21 Aprili 1926, huko London

image
na Radio Jambo

Habari09 September 2022 - 09:26

Muhtasari


• Katika miaka yake ya mapema, hakuna mtu ambaye angeweza kutabiri kwamba kiti cha ufalme kingekuwa hatima yake.

Malkia Elizabeth II aliishi maisha yake akiangaziwa pakubwa . Tunatazama nyuma katika enzi yake, kutoka akiwa mtoto hadi mrithi mtawala wa kifalme aliyetawala muda mrefu zaidi wa Uingereza.

Elizabeth Alexandra Mary Windsor alizaliwa tarehe 21 Aprili 1926, katika nyumba karibu na Berkeley Square huko London. Alikuwa mtoto wa kwanza wa Albert, Duke wa York - mtoto wa pili wa George V - na mkewe, Lady Elizabeth Bowes-Lyon wa zamani.

Katika miaka yake ya mapema, hakuna mtu ambaye angeweza kutabiri kwamba kiti cha ufalme kingekuwa hatima yake.

Hata hivyo, ilisemekana kuwa alionyesha hisia ya ajabu ya uwajibikaji tangu umri mdogo sana.

Elizabeth na dada yake, Margaret Rose, aliyezaliwa mwaka wa 1930, walisoma nyumbani.

Kufuatia kusalimisha kiti cha ufalme na Mfalme Edward VIII mnamo 1936, babake Elizabeth alikua George VI na akawa mrithi.

Wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu, Elizabeth na dada yake Margaret walihamishwa hadi Windsor. Picha hii inawaonyesha wakitangaza kwa taifa katika kipindi cha Children's Hour kwenye idhaa ya BBC.

Binti wa kifalme alijiunga kwa muda mfupi na Huduma ya Auxiliary Territorial Service (ATS) mwishoni mwa vita alipojifunza kuendesha gari na kuyafanyia ukarabati.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved