logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ababu Namwamba avunja kimya baada ya kuteuliwa kuwa waziri wa michezo

"Shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Rais William Ruto

image
na Radio Jambo

Yanayojiri27 September 2022 - 19:40

Muhtasari


  • mbunge huyo wa zamani wa eneo bunge la Budalangi alijawa na shukrani nyingi kwa mkuu wa nchi kwa kumteua katika baraza lake la mawaziri

Aliyekuwa katibu mkuu wa utawala (CAS) katika utawala wa rais wa zamani Uhuru Kenyatta Bw Ababu Namwamba amejitokeza kutoa taarifa yake ya kibinafsi kufuatia hatua ya rais William Ruto kumteua nafasi ya juu serikalini.

Katika taarifa yake kwenye mitandao ya kijamii, mbunge huyo wa zamani wa eneo bunge la Budalangi alijawa na shukrani nyingi kwa mkuu wa nchi kwa kumteua katika baraza lake la mawaziri.

Namwamba aliteuliwa kuwa waziri katibu ajaye wa masuala ya vijana, michezo na sanaa katika kile kitakachomfanya achukue wadhifa huo kutoka kwa balozi Amina Mohamed ambaye amekuwa akihudumu katika wadhifa sawia katika awamu ya mwisho ya utawala wa Uhuru Kenyatta.

"Shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Rais William Ruto kwa imani na imani ya kuniteua kuwa Waziri wa Masuala ya Vijana, Michezo na Sanaa," aliandika.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved