Sakaja awashauri abiria kuchagua kati ya matatu ya muziki au ile tulivu kabla ya kuabiri
Alisema mambo ya grafitti na muziki kubwa sio upuzi bali ni utamaduni wa jiji
• Alisema iwapo hupendi kelele basi subiri gari ambali halina sauti.
• Sakaja pia alisema anaunga mkono wahudumu wa matatu walioweka grafiti kwenye magari yao.
Gavana wa Nairobi Johnson Sakaja amepuuzilia mbali malalamishi yaliotolewa kwake kuwazima wahudumu wa magari ya umma wanaoweka sauti ya juu ya muziki kwenye magari yao.
Sakaja alisema anaunga mkono wahudumu wa matatu ambao pia walioweka grafiti kwenye magari yao akisema huo ni urembo na ni utamaduni wa Nairobi.
"Eti mambo ati graffiti na muziki kwa matatu ati ni mbaya, hio ni ufala. Huu ni utamaduni wetu." alisema Sakaja.
Gavana alisema madereva wana uhuru wa kuchora magari yao na kujiamulia kinachowafaa wasafiri.
"Kama mtu anataka matatu haina muziki angojee aingie yenye haina muziki na kama mtu anataka kusema iko na ngoma aingie yenye iko na ngoma," Sakaja alisema.
Zaidi ya hayo Sakaja aliongeza kuwa atakuwa anawapiga jeki na kuwapa tuzo wahudumu wa matatu pamoja na Saccos zinazofanya vizuri kwa kuzingatia nidhamu.
Katika utawala wa aliyekuwa rais mustaafu Uhuru Kenyatta alikuwa ameiamuru halmashauri ya NTSA kuruhusu michoro kwenye matatu zao.
NTSA hata hivyo ilionya dhidi ya matumizi ya michoro inayouudhi na kuchukiza au maneno yanayochukiza pamoja na picha au ishara.