logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Tudumishe amani nchini,'Ruto awaambiwa wapinzani wake

Alisema upinzani haufai kuwafukuza Wakenya dhidi ya wenzao.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri28 November 2022 - 09:59

Muhtasari


  • Rais alizungumza wakati wa uzinduzi wa vyakula vya Twiga kwenye mji wa Tatu siku ya Jumatatu

Rais William Ruto amewaambia wanachama wa upinzani wakiongozwa na kiongozi wa ODM Raila Odinga kukosoa utawala wake wanavyotaka lakini kudumisha amani.

"Nataka kuwaambia ndugu zetu wa upinzani, ukosoe kila unapotaka, lakini tuiweke nchi yetu kwa amani," alisema.

Rais alizungumza wakati wa uzinduzi wa vyakula vya Twiga kwenye mji wa Tatu siku ya Jumatatu.

Alisema upinzani haufai kuwafukuza Wakenya dhidi ya wenzao.

Siku ya Jumapili, Raila alisema watafanya mikutano kote nchini kutafuta maoni kutoka kwa umma kuhusu ombi la kuwaondoa makamishna wanne wa IEBC.

 "Mikutano ya hadhara itaanza katika miji mikuu na kuenea katika miji mingine," alisema.

Mkutano wa kwanza utafanyika Nairobi na wa pili na wa tatu utafanyika Mombasa na Nakuru mtawalia.

"Nataka kuzungumzia suala muhimu la makamishna wa IEBC. Tutashauriana sana na watu wa Kenya. Tutaanza Nairobi Jumatano," Raila alisema.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved