logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raila amwomba Kingi aruhusu Azimio kufanya mabadiliko ya uongozi katika Seneti

Raila aliteta kuwa Bunge halina shughuli ya kutumbuiza maagizo ya mahakama.

image
na

Makala07 March 2023 - 14:30

Muhtasari


  • Alisisitiza kuwa vyama vya siasa viruhusiwe kufanya mabadiliko ya uongozi wao ndani ya Bunge bila kuingiliwa

Kiongozi wa Azimio Raila Odinga amemtaka Spika wa Seneti Amason Kingi kuruhusu upande wa Wachache kuwa na uongozi unaotaka katika Bunge.

Akizungumza na vyombo vya habari katika majengo ya Bunge, Raila alisema Kingi anafaa kuwaachia upinzani kuwa na uongozi unaotaka katika Bunge hilo.

“Tuna changamoto za uongozi katika Seneti. Uongozi wa vyama vya siasa usiingiliwe,” alisema.

Alishangaa ni kwa nini Kingi bado hajafanya mabadiliko katika Seneti licha ya Azimio kupata viongozi wapya katika Bunge hilo.

Alisisitiza kuwa vyama vya siasa viruhusiwe kufanya mabadiliko ya uongozi wao ndani ya Bunge bila kuingiliwa.

“Chama cha siasa kinapofanya mabadiliko yake, hakipaswi kuingiliwa. Tunamwomba Spika au mtu mwingine yeyote kuruhusu Azimio la Umoja-One Kenya Alliance kufanya mabadiliko katika uongozi wake wapendavyo,” akasema.

Pamoja naye walikuwa maseneta Ledama Ole Kina (Narok), Enock Wambua (Kitui) na Edwin Sifuna (Nairobi).

Raila aliteta kuwa Bunge halina shughuli ya kutumbuiza maagizo ya mahakama.

Fatuma Dullo (Isiolo) ambaye alikuwa ameteuliwa kung’olewa kwenye nafasi ya Mnadhimu wa Walio wachache alihamia Mahakama ya Mizozo ya Vyama vya Siasa (PPDT) akipinga uamuzi wa Azimio kumwondoa katika nafasi hiyo.

Maandamano ya Raila yanakuja baada ya Kingi kukosa kutangaza mabadiliko ya uongozi katika Bunge.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved