logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Meru: Wafanyikazi wa kaunti kushiriki ibada ya maombi mara tatu kwa wiki

Gavana Mwangaza ambaye ni mchungaji alitangaza kuwa ibada hiyo itaanza Machi 13.

image
na Radio Jambo

Makala13 March 2023 - 09:19

Muhtasari


• Maombi hayo yatakuwa yanafanyika mara tatu kwa wiki, Jumatatu, Jumatano na Ijumaa katika chumba cha mikutano cha kaunti hiyo.

Gavana wa Meru akiombewa

Gavana wa kaunti ya Meru Kawira Mwangaza ametangaza ratiba mpya ya maombi kwa wafanyikazi wote wa kaunti hiyo ambayo itaanza kutekelezwa kuanzia Jumatatu tarehe 13, ambayo ni leo.

Kupitia bango ambalo gavana huyo aliyenusurika kutimuliwa madarakani alipakia kwenye ukurasa wake wa Facebook, sasa ni rasmi kwamba wafanyikazi wote wa kaunti walashiriki ibada ya maombi kila Jumatatu, Jumatano na Ijumaa kila wiki.

Kulingana na ratiba hiyo, ibada ya maombi itakuwa inafanyika katika chumba cha mikutano cha kaunti hiyo na kuanzia saa moja kasoro robo hadi saa moja kamili asubuhi, itakuwa ni nyimbo za sifa na ibada.

Saa Moja kamili hadi saa moja na robo ni maombi yatakayokuwa yakiongozwa huku kuanzia saa moja na robo hadi saa moja na nusu itakuwa ni mahubiri.

Taarifa hii inakuja siku chache tu baada ya taarifa nyingize ambazo hata hivyo hazikudhibitishwa kutoka ikulu kwamba rais Ruto amewaagiza wafanyikazi wa ikulu kushiriki maombi katika siku teule za wiki.

Baadhi ya watu waliotoa maoni yao katika tangazo hilo la gavana Mwangaza walimtaka hata hivyo asiweke shuruti kwa ratiba hiyo na maombi yawe ni jambo la kujitolea tu kwa wafanyikazi.

“Ilimradi haufanyi kuwa jambo la lazima. Usianze kugombana na wafanyikazi wa kaunti wanaokosa vipindi hivyo vya maombi. Kila Mkenya ana uhuru wa kuabudu. Wanaweza kuchagua kuwa wa madhehebu ya kidini unayojiandikisha, au wanaweza kuchagua kutoshiriki,” Lewis Kithinji Mugambi alisema.

Wengine walimpongeza kwa hilo wakisema kwamba ndio uamuzi wa njia sahihi kutanguliza maombi katika kila hatua.

“Mheshimiwa Gavana Mh Kawira Mwangaza kwa maombi kila kitu kinawezekana tunaamini... Lakini Gavana wangu wa Kaunti ya Meru sisi wa imani tofauti tunafikiria kuwaalika wengine,” mwingine alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved