logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Homa Bay: Mhubiri wa miaka 45 akamatwa kwa kunajisi msichana wa gredi 4

Kamanda wa polisi aliwataka watu kujihusisha kimapenzi na watu wa rika lao.

image
na Radio Jambo

Makala15 March 2023 - 11:53

Muhtasari


• Mchungaji huyo pamoja na msichana huyo mwathiriwa ambaye alikuwa anasoma gredi 4 wote wanatoka katika kijiji kimoja.

Polisi katika kaunti ya Homa Bay wamemweka chini ya ulinzi kasisi wa kanisa moja mwenye umri wa miaka 45 kwa tuhuma za kumnajisi msichana wa miaka 16.

Inadaiwa kwamba kasisi huyo alimfanyia kitendo cha aibu msichana huyo nyumbani kwake usiku wa Jumapili wakati wa ibada ya maombi.

Mchungaji huyo pamoja na msichana huyo mwathiriwa ambaye alikuwa anasoma gredi 4 wote wanatoka katika kijiji kimoja.

Kamanda wa polisi katika kaunti ndogo ya Homa Bay Sammy Koskei katika video moja iliyopakiwa mitandaoni alidhibitisha kisa hicho na kusema kwamba uchunguzi Zaidi kubaini mazingira yaliyosababisha tukio hilo la aibu umeanzishwa.

“Tunachunguza kisa cha unajisi kilichojiri Machi 11 katika sehemu inayojulikana kama Kapita, mpaka sasa tumefanikiwa kumtia nguvuni mshukiwa, mchungaji wa kanisa liitwalo Roho, mwenye umri wa miaka 45 na alimnajisi msichana wa miaka 16 na kesi hiyo iko mahakamani,” Kamanda huyo alisema huku akitoa ushari kwa watu wa kaunti ya Homa Bay kutojihusisha katika vitendo vya mapenzi na watoto wadogo na badala yake kujihusisha kimapenzi na watu wa rika lao.

Afisa wa watoto katika kaunti ndogo ya Homa Bay Joseph Otieno alisema mama wa mwathiriwa alimwasilisha kwa maombi na kuwaacha peke yao katika hekalu hilo. Ni wakati huu ambapo mchungaji anadaiwa kumnajisi msichana huyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved