logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Polisi wawakamata washukiwa 3 kwa wizi wa Milioni 8 katika kituo cha mafuta

polisi walisema pesa hizo ziliibiwa katika kituo cha mafuta ya petroli huko Kinangop, Nyandarua.

image
na

Makala23 May 2023 - 10:13

Muhtasari


• Washukiwa hao wanadaiwa kuingia ndani ya jengo hilo kupitia paa kabla ya kuziiba pesa hizo baada ya kuvunja sefu.

• Washukiwa hao waliotambulika kama David Mushendu, Moses Cherish na Eliud Wangai walipatikana na kima cha shinlingi milioni 2.5.

Kituo cha pampu ambapo pesa hiizo zinadaiwa kuibwa.

Polisi wamewakamata washukiwa 3 kuhusiana na kutoweka kwa milioni 8 zilizoibwa kutoka kwa mfanyabiashara wa Kiambu.

Katika taarifa ya idara ya upelelezi na makosa ya jinai (DCI) kwenye akaunti yake ya Facebook polisi walisema pesa hizo zilizokuwa zimetoweka mwezi mmoja uliopita, ziliibiwa katika kituo cha mafuta ya petroli huko Kinangop, Nyandarua.

Washukiwa hao wanadaiwa kuingia ndani ya jengo hilo kupitia paa kabla ya kuziiba pesa hizo baada ya kuvunja sefu.

“Katika kisa hicho kilichoripotiwa mwishoni mwa mwezi uliopita na mke wa mfanyabiashara huyo, pesa hizo ziliibwa kwenye sefu iliyofichwa katika kituo cha mafuta kilichotelekezwa kilicho Kinangop, Nyandarua,” sehemu ya taarifa hio ilisoma.

Washukiwa hao waliotambulika kama David Mushendu, Moses Cherish na Eliud Wangai walipatikana na kima cha shinlingi milioni 2.5.

“Jumla ya Sh2.5 milioni zimepatikana kutoka kwa washukiwa,” taarifa hiyo ilisoma.

Washukiwa hao wanakabiliwa na kesi ya wizi kinyume na kifungu cha 281 cha kanuni ya adhabu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved