In Summary
  • Atwoli aliitisha kikao cha bodi siku ya Jumanne. Amekuwa nje ya nchi kwa muda na alirejea Jumapili.
Katibu mkuu wa Muungano wa Vyama vya Wafanyakazi (COTU) Francis Atwoli
Image: TWITTER

Katibu mkuu wa Muungano wa Vyama vya Wafanyakazi (COTU) Francis Atwoli ametoa rambi rambi kwa mwenyekiti marehemu Rajabu Mwondi.

Kulingana na Atwoli ambaye aliongoza bodi ya Cotu kumkumbuka Mwondi, alisema chama cha wafanyakazi kilipoteza mtu aliyekuja, kuona na kushinda.

Aliendelea kueleza Mwondi kama kiongozi na rafiki wa kweli, ambaye amemshauri katika safari yake kama mwana chama cha wafanyakazi.

Atwoli aliitisha kikao cha bodi siku ya Jumanne. Amekuwa nje ya nchi kwa muda na alirejea Jumapili.

"Leo asubuhi, niliongoza kikao cha Halmashauri Kuu ya @COTU_K na Makatibu Wakuu Washirika katika kutoa heshima kwa Mwenyekiti Mkuu wa COTU (K) Rajabu Wellingtone Mwondi. Mwondi hakuwa tu ndugu au kiongozi, alikuwa rafiki wa kweli. , mshauri, na mwanga wa kuniongoza katika safari yangu yote katika vuguvugu la wafanyikazi. Nitamkosa kabisa Mwenyekiti Rajabu Wellington Mwondi. Tumempoteza mtu mashuhuri. Mtu aliyekuja, kuona na kushinda," Cotu SG alisema.

Mwondi alifariki Agosti 16, alipokuwa akipatiwa matibabu katika hospitali ya Nairobi.

Alihudumu kama mwenyekiti wa Cotu kwa zaidi ya miongo miwili.

Katika ujumbe wake wa awali, Atwoli alimtaja Mwondi kama Mwenyekiti aliyejitolea, ambaye alitetea bila kuchoka malipo ya haki, mazingira salama ya kazi, na ustawi wa jumla wa wanachama wa Muungano.

"Hekima yake, huruma, na juhudi zisizo na uchovu zimebadilisha maisha ya wafanyikazi wengi, na kuinua shirika letu hadi viwango vipya. Uongozi wake ulivuka mipaka ya wakati, na kuacha alama isiyoweza kufutika katika historia ya COTU (K)," Atwoli alisema.

 

 

 

View Comments