logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gavana Wavinya Ndeti amsihi Rais Ruto kushughulikia bei ya juu ya mafuta

"Tutawalishaje watoto hawa? Hatuwezi kukaa kimya kuhusu hilo.

image
na Radio Jambo

Makala17 September 2023 - 13:43

Muhtasari


  • Hii ni huku kukiwa na lawama kutoka kwa umma na viongozi sawa dhidi ya kuongezeka kwa gharama ya mafuta ambayo inatishia kuyumba katika sekta mbalimbali za uchumi.

Gavana wa Machakos Wavinya Ndeti amemtaka Rais William Ruto kutafuta suluhu mwafaka ili kuwaepusha Wakenya kutokana na athari mbaya ya kupanda kwa bei ya mafuta.

Hii ni huku kukiwa na lawama kutoka kwa umma na viongozi sawa dhidi ya kuongezeka kwa gharama ya mafuta ambayo inatishia kuyumba katika sekta mbalimbali za uchumi.

Kulingana na Gavana wa Machakos, gharama ya mafuta inapopanda, gharama za usafiri huongezeka hali ambayo hupanda bei ya bidhaa muhimu kama vile chakula na bidhaa nyingine za matumizi, hivyo basi kuwaelemea zaidi kaya za Kenya ambazo tayari zinatatizika kujikimu kimaisha.

"Tutawalishaje watoto hawa? Hatuwezi kukaa kimya kuhusu hilo. Maisha yanazidi kuwa magumu kwa kila mtu," Wavinya alieleza wakati wa hafla ya kanisani Jumamosi.

Gharama ya mafuta nchini Kenya ilifikia rekodi ya juu siku ya Ijumaa ikivuka alama ya Shilingi 200 kwa mara ya kwanza. Hili limeibua kengele kote nchini, hali iliyowafanya wananchi kuhoji ni vipi wataweza kukabiliana na kupanda kwa gharama za maisha.

Jumapili naibu Rais alivunja kimya chake kuhusu bei ya juu ya mafuta huku akisema kwamba imeongezeka ulimwenguni kote na kuwasihi Wakenya wawe wavumilivu.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved