logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Huzuni!Mwanamume aaga dunia siku ya harusi yake Kangundo

Kisha familia ilienda kwa mapokezi katika Shule ya Msingi ya Kamanzi iliyo karibu.

image
na Radio Jambo

Habari17 September 2023 - 09:33

Muhtasari


  • Mary Musyoki alipaswa kufanya upya viapo vyake vya harusi na mumewe, Michael katika Kanisa Katoliki la Kamanzi Kaunti ya Machakos.
crime scene

Mwanamke mmoja ambaye alitarajiwa kurejelea viapo vyake  vya ndoa siku ya Jumamosi aliachwa mjane baada ya mume wake kuanduka kwenye bafu alipokuwa akioga kujiandaa kwa ajili ya siku yake ya kipekee..

Mary Musyoki alipaswa kufanya upya viapo vyake vya harusi na mumewe, Michael katika Kanisa Katoliki la Kamanzi Kaunti ya Machakos.

Michael alikimbizwa hospitalini lakini alitangazwa kuwa amefariki alipofika.

Mary akizungumza na vyombo vya habari siku ya JUmamose alisema kuwa;

"Alianguka alipokuwa anaoga kujitayarisha, tulimpeleka hospitali lakini alitangazwa kuga dunia baada ya kufika."

Mwili wake ulipelekwa kwa makafani  ya Kivaani na familia ikarejea nyumbani kujiandaa kwenda kanisani licha ya mkasa huo.

Sherehe hiyo ilipaswa kuwa upya wa viapo pamoja na uthibitisho wa kanisa.

Misa hiyo iliongozwa na Fr Jones Muinde.

Kisha familia ilienda kwa mapokezi katika Shule ya Msingi ya Kamanzi iliyo karibu.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved