In Summary
  • Alisema hakukuwa na majeraha ya ulinzi akimaanisha mtu huyo alikuwa amelala huku akichomwa kisu.
  • Mshambuliaji hakuiba chochote kutoka kwa nyumba ya marehemu, polisi walisema.

Mkurugenzi wa fedha wa Nairobi Hospital Erick Maigo alikuwa na majeraha 25 ya kuchomwa visu na kusababisha kifo chake, uchunguzi wa maiti unaonyesha.

Uchunguzi wa upasuaji wa maiti ambao ulifanywa katika Jumba la kuhifadhi maiti la Lee mnamo Jumamosi ulifichua baadhi ya viungo muhimu vilinyakuliwa na visu kwenye shambulio hilo.

“Tulipiga hesabu na kukuta alikuwa na majeraha 25 ya kuchomwa kisu. Hili lilisababisha kuvuja damu nje na ndani,” akasema mtaalamu mkuu wa serikali Dkt Johansen Oduor

 

Alisema hakukuwa na majeraha ya ulinzi akimaanisha mtu huyo alikuwa amelala huku akichomwa kisu.

Mshambuliaji hakuiba chochote kutoka kwa nyumba ya marehemu, polisi walisema.

Maigo, 36 alipatikana Ijumaa asubuhi akiwa ameuawa katika nyumba yake eneo la Woodley, Nairobi. Mwili wa Maigo ulipatikana na visu 25 dakika chache baada ya kuuawa mwendo wa saa kumi na mbili asubuhi, polisi walisema.

Mshambulizi wake, mwanamke ambaye labda alikuwa amelala nyumbani kwake alitoroka dakika chache kabla ya polisi kufika.

Hakuna aliyekamatwa hadi sasa. Polisi walikuwa wamehesabu majeraha 16 ya visu kwenye eneo la tukio lakini uchunguzi wa maiti ulithibitisha kuwa walikuwa 25.

"Hii iliendeshwa na hasira au kitu kingine. Bado hatujajua,” afisa mmoja anayefahamu uchunguzi huo alisema

Familia yake ilihudhuria zoezi la upasuaji wa maiti Majirani katika ghorofa ya Woodley Annex walisema walimsikia Maigo akiugua kwa maumivu. Waliamua kuuendea mlango wake na kuugonga ndipo akakutana na mwanamke mmoja ambaye aliwajulisha kuwa kila kitu kilikuwa sawa na alikuwa anatafuta funguo ili afungue.

Mwanamke huyo alichungulia dirishani akidai kuwa hakuweza kupata ufunguo. Majirani walimsikia Maigo akiwa bado anaugulia maumivu na kutafuta msaada.

Bibi aliyekuwa ndani ya nyumba hiyo alikataa kufungua na kuwafanya majirani kuwatahadharisha usalama katika boma hilo. Waliwaomba wanausalama wasiruhusu mtu yeyote kutoka katika nyumba hiyo kuondoka.

Kulingana na polisi, walikimbilia katika kituo cha polisi cha Kibra ambapo walitoa ripoti ya shughuli za kutiliwa shaka katika nyumba hiyo.

Wakati polisi walipofika eneo la tukio, walimkuta mwanamke huyo alipatikana hayupo.

View Comments