logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kiambu: Mwanamume apigwa na umeme hadi kufa akijaribu kumuibia bosi wake kahawa

“Wakati alipokuwa anaondoka katika kiwanda, aligusa nyaya ya umeme."

image
na Radio Jambo

Makala16 November 2023 - 08:53

Muhtasari


• Baada ya uchunguzi wa kina, walibaini kwamba jamaa huyo alikwenda kwa lengo la kuiba kahawa za mwajiri wake.

Mtambo wa nyaya za stima

Mwanamume mmoja amefariki kwa kupigwa na umeme akiwa katika mchakato wa kuvizia kahawa na bosi wake kwa lengo la kuiiba.

Kwa mujibu wa Nation, jamaa huyo wa umri wa makamo alitambulika kama Evans Njoroge alipatikana amekauka katika mtaro ambako alikuwa anavizia kahawa hiyo ambayo ilikuwa imewekwa ili kukauka.

Polisi walipofika kwenye eneo la tukio, walimpata marehemu na kand yake nusu gunia ya kahawa hizo ambazo anashukiwa alikuwa katika harakati za kuiba.

Baada ya uchunguzi wa kina, walibaini kwamba jamaa huyo alikwenda kwa lengo la kuiba kahawa za mwajiri wake.

“Wakati alipokuwa anaondoka katika kiwanda, aligusa nyaya ya umeme ambayo imetumika kama ua la kuzunguka kiwanda hicho na hapo ndipo alianguka kwenye mtaro,” repoti ya polisi ilisoma.

Mwili wake uliondolewa sehemu hiyo na kusafirishwa hadi makafani ya Kigumo kwa uchunguzi Zaidi.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved