logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu wenye alama ya D+ kwenye KCSE hawatapata nafasi ya kuajiriwa kuwa polisi nchini

Kamati ya kushughulikia mabadiliko katika idara ya polisi inapendekeza alama ya chini kuwa C-.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri19 November 2023 - 07:17

Muhtasari


• “Ili kutatua suala la kutokomaa kiakili ambalo limekuwa likionekana kwa makurutu wapya, umri wa chini unastahili kupandishwa kutoka miaka 18 hadi 21,” jopokazi hilo lilisema.

KDF kuajiri mwezi ujao,

Kikosi Kazi cha Kitaifa kuhusu Marekebisho ya Polisi kimetoa mapendekezo muhimu ya kuajiri maafisa wa siku zijazo katika Huduma ya Kitaifa ya Polisi na Huduma ya Magereza ya Kenya.

Muhimu kati ya mapendekezo haya ni kwamba sifa za kitaaluma za wanaotaka kujiandikisha zipandishwe kutoka daraja la sasa la chini kabisa la KCSE la D plus hadi C minus.

Katika mapendekezo yake, jopokazi hilo linaloongozwa na jaji mkuu mstaafu David Maraga lilisema kuinua sifa za kuajiri kutaongeza weledi katika utumishi wenye nidhamu.

“Jopokazi hili linapendekeza kiwango cha chini cha mtu kuruhusiwa kuajiriwa katika idara ya polisi kupandishwa hadi C- kutoka  D+ katika mtihani wa KCSE,” sehemu ya taarifa hiyo ilisoma.

Hata hivyo, Maraga na wenzake katika pendekezo hilo ambalo waliwasilisha kwa rais mwishoni mwa juma, walipendekeza kuwa wale kutoka maeneo yanayohisi kutengwa wapewe nafasi ya kuingia jeshini ya alama ya D+

Kando na pendekezo hilo la kiwango cha alama, jopokazi hilo pia lilipendekeza muda wa kufunzwa kwa makurutu kuongezwac hadi miezi 12 kutoka kwa miezi 9 ya sasa.

Na pia walipendekeza umri wa chini kupandishwa kutoka miaka 18 hadi miaka 21 ili kusuluhisha suala la kutokomaa.

“Ili kutatua suala la kutokomaa kiakili ambalo limekuwa likionekana kwa makurutu wapya, umri wa chini unastahili kupandishwa kutoka miaka 18 hadi 21,” jopokazi hilo lilisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved