In Summary

• Afisa huyo anadaiwa kudokezewa kuhusu mkewe na kasisi kuwa katika uhusiano na akavizia nyumbani kwake na kuingia katika chumba kimoja bila ya mkewe kujua.

Mke aomba kufanya mapenzi na ex kabla kufa
Image: Hisani

Hali ya simanzi ilitanda katika kijiji kimoja huko Kapsabet kaunti ya Nandi baada ya afisa wa KDF kudaiwa kumuua kasisi wa kanisa la ACK baada ya kile kilichotajwa kuwa ni fumanizi.

Kwa mujibu wa taarifa, afisa huyo alirejea nyumbani kinyemela nyakati za usiku na kumfumania mtumishi wa Mungu, mwenye umri wa miaka 43 katika kitanda chake na mke wake wakishiriki mapenzi kabla ya kumpiligia misumari kwenye uti wa mgongo na kumkata uume wake.

Afisa huyo anadaiwa kudokezewa kuhusu mkewe na kasisi kuwa katika uhusiano na akavizia nyumbani kwake na kuingia katika chumba kimoja bila ya mkewe kujua.

Inasemekana alisubiri kwa hadi saa 2 hivi ili wawili hao kuingia kitandani na kuwafumania ambapo alimshambulia kwa adhabu kali zilizopelekea umauti wake baadae hospitalini.

Kisha afisa huyo aliyekasirika akamgeukia mke wake, akiuvunja mkono wake, kisha akapigilia misumari kwenye uti wa mgongo wa kasisi.

Majirani waliambia The Star kuwa afisa huyo alimweka mke kwenye kona ya chumba cha kulala huku akimchinja mpenzi wake kwa kumkata sehemu zake za siri huku akitazama.

Mpiga simu ambaye jina lake halikufahamika alifahamisha polisi kuhusu ghasia hizo mwendo wa saa tatu asubuhi Alhamisi, kamanda wa polisi wa Nandi Dickens Njogu alisema.

 

"Ilikuwa tu asubuhi ya leo wakati Mkuu wa Kanisa Kuu la St Barnabas Mchungaji Nillah Bassy alipokuja kutoa ripoti rasmi ya tukio hilo la kusikitisha ambalo maafisa wa polisi walihamia," afisa huyo alisema.

Majirani walimkimbiza Rev Kemei katika hospitali ya Kapsabet Level 5 akiwa katika hali mahututi. Alirejelewa Eldoret, ambapo alitangazwa kuwa amefariki alipofika katika Hospitali ya Top Hill.

View Comments