In Summary
  • Kulingana na Karua, ataendelea kusimama na Wakenya na kuwatumikia kama kiongozi wao wa upinzani bila kujali mabadiliko ya kisiasa yanayoendelea.
Martha Karua

Kiongozi wa chama cha NARC-Kenya Martha Karua mnamo Alhamisi alipuuzilia mbali hatua inayowezekana ya kujiunga na utawala wa Rais William Ruto.

Akizungumza wakati wa Mahojiano mkuu wa Azimio alifafanua kuwa bado yuko kwenye upinzani licha ya mgawanyiko unaojitokeza ndani ya muungano huo.

Kulingana na Karua, ataendelea kusimama na Wakenya na kuwatumikia kama kiongozi wao wa upinzani bila kujali mabadiliko ya kisiasa yanayoendelea.

"Nachukua upinzani. Kinachonifaa ni kusimama na Wakenya na nitasimama nao wakati wote lakini nikipata nafasi ya kuwahudumia, nitawahudumia,” Karua alisema.

“Sitarudi nyuma. Nitaendelea kueleza msimamo wangu wa kisiasa. Iwapo fursa itapatikana iwe serikalini au kwa upinzani.”

Aidha Karua ametoa wito kwa vijana kuendelea kupigania uongozi bora kwa ajili ya kuboresha taifa. Kulingana na Karua, hakukuwa na dalili za kujisalimisha kwa kizazi kipya.

Kiongozi huyo wa NARC-Kenya alishutumu wanasiasa kwa kupuuza lalama zilizotolewa na waandamanaji hao vijana.

"Injini ya mapinduzi daima ni vijana, inaweza kuongozwa na wengine lakini ni vijana ambao huwa mbele kila wakati," Karua alifichua.

Kauli ya Martha Karua inakuja huku kukiwa na madai ya mgawanyiko ndani ya Muungano wa Azimio baada ya baadhi ya wanasiasa kuchagua kufanya kazi na Rais William Ruto.

 

 

 

 

 

View Comments