In Summary

•KPLC imesema baadhi ya maeneo ya kaunti sita za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

•Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Kiambu, Makueni, Trans Nzoia, Kakamega, Laikipia, na Kilifi.

Kenya Power
Image: HISANI

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumanne, Julai 30. 

Katika taarifa ya Jumatatu jioni, kampuni hiyo ilisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyiwa kwenye mitambo.

Walisema baadhi ya maeneo ya kaunti sita za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni. Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Kiambu, Makueni, Trans Nzoia, Kakamega, Laikipia, na Kilifi.

Katika kaunti ya Kiambu, sehemu kadhaa za eneo la Gikambura zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Baadhi ya sehemu za eneo la Kaumoni katika kaunti ya Machakos zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Sehemu za maeneo ya Endebes na Panacol katika kaunti ya Trans Nzoia zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa saba mchana.

Katika kaunti ya Kakamega, maeneo ya Samitsi na Kalenda yataathirika kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Wakati huohuo, sehemu za eneo la Chasimba katika kaunti ya Kilifi pia zitakosa umeme.

Baadhi ya sehemu za maeneo ya Makutano na Katheri katika kaunti ya Laikipia zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

View Comments