logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bei ya mafuta yaongezeka kwa shillingi 3.40

Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Petroli nchini(EPRA) imetangaza kuongeza bei ya  mafuta nchini.

image
na

Yanayojiri15 May 2023 - 04:46

Muhtasari


•Ongezeko hili linamaanisha bei ya petroli imeongezeka hadi shilingi 182.70, ile ya dizeli ikipanda hadi 168.40 na mafuta taa yatauzwa kwa shilingi 161.13 jijini Nairobi.

Mamlaka ya Kudhibiti Nishati na Petroli nchini (EPRA) imetangaza kuongeza bei ya  mafuta nchini.

Katika mabadiliko hayo, bidhaa hio mihimu imeongezeka kwa shilingi 3.40 kwa lita ya petroli, shillingi 6.40 kwa mafuta ya dizeli na shillingi 15.19 kwa lita moja ya mafuta ya taa.

Ongezeko hili linamaanisha bei ya petroli imeongezeka hadi shilingi 182.70, ile ya dizeli ikipanda hadi 168.40 na mafuta taa yatauzwa kwa shilingi 161.13 jijini Nairobi.

“Kwa mujibu wa Kifungu cha 101(y) cha Sheria ya Petroli ya 2019 na Notisi ya Kisheria Na.192 ya 2022,EPRA imepania kubadilisha bei za juu zaidi za rejareja na za jumla za bidhaa za petroli ambazo zitaanza kutumika kuanzia tarehe 15Mei hadi tarehe 14 Juni 2023.” Taarifa hio ilisoma.

Bei hizo ni pamoja na asilimia 8 ya ushuru wa Ongezeko la Thamani ya bidhaa (VAT)

Katika taarifa kwenye vyombo vya Habari, mamlaka hiyo iliashiria ongezeko hilo ni baada ya kuzingatia uzani wa wastani wa gharama ya bidhaa za petroli iliyosafishwa kutoka nchi za nje.

Bei mpya zilianza kutumika saa sita usiku wa kuamkia Jumatatu, Mei 14 hadi saa sita usiku wa Juni 14, 2023.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved