logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Fahamu maeneo ya Kenya ambako hakutakuwa na stima leo, Novemba 2

KPLC imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Alhamisi.

image
na Radio Jambo

Makala02 November 2023 - 04:31

Muhtasari


•KPLC ilitangaza kuwa maeneo kadhaa katika kaunti 4 za Kenya yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni

•Kukatizwa kwa umeme katika maeneo yaliyotajwa kumepangwa kwa sababu ya shughuli za matengenezo zitakazokuwa zikifanyika.

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Alhamisi.

Katika taarifa ya Jumatano jioni, kampuni hiyo ilitangaza kuwa maeneo kadhaa katika kaunti 4 za Kenya yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni. Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Nairobi,Nyandarua, Kilifi na Mombasa.

Katika kaunti ya Nairobi, sehemu za eneo la Riverside zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni. Aidha, sehemu za mtaa wa Westlands na Parklands Rd zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa nane alasiri.

Sehemu za mtaa wa Tudor katika kaunti ya Mombasa zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni siku ya Alhamisi.

Wakati huo huo, sehemu za maeneo ya Kokotoni na Jimba katika kaunti ya Kilifi yatashuhudia kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Katika kaunti ya Nyandarua, mji mzima wa Engineer utaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

KPLC imeeleza kuwa kukatizwa kwa umeme katika maeneo yaliyotajwa kumepangwa kwa sababu ya shughuli za matengenezo zitakazokuwa zikifanyika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved