logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Miguna Miguna afichua sababu kuu ya kwenda Kisumu Ijumaa

Miguna alisema itakuwa ziara ya heshima kwani hajakutana na familia yake kwa muda mrefu.

image
na Radio Jambo

Habari26 October 2022 - 16:14

Muhtasari


  • "Kwenda nyumbani, haswa kwa mtu aliyehamishwa kwa nguvu kwa miaka 5, sio kitendo cha vita. Ni kitendo cha amani, urejesho wa kihemko na kimwili," alisema.
Jenerali Miguna hatimaye ametua nchini

Wakili Miguna Miguna anatazamiwa kuzuru nyumbani kwake Kisumu siku ya Ijumaa baada ya kurejea kutoka Kanada alikokuwa uhamishoni kwa lazima.

Miguna alisema itakuwa ziara ya heshima kwani hajakutana na familia yake kwa muda mrefu.

"Kwenda nyumbani, haswa kwa mtu aliyehamishwa kwa nguvu kwa miaka 5, sio kitendo cha vita. Ni kitendo cha amani, urejesho wa kihemko na kimwili," alisema.

Aliwasihi wapinzani wake wasitume wahuni wampige mawe kwani anaenda kuwaomboleza wanafamilia wake walioaga dunia alipokuwa hayupo.

"Tafadhali msiwahamasishe vijana wasio na ajira kunipiga mawe siku ya Ijumaa. Naenda kuomboleza wanafamilia wangu," alisema.

Miguna alikuwa tayari ametangaza Jumanne kwamba atazuru nyumbani kwake.

Katika taarifa yake, wakili huyo alisema atakuwa katika kijijini Kisumu Ijumaa, Oktoba 28.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved