logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Siku moja utakuwa naibu wangu-Babu Owino amwambia Charlene Ruto

Ameonekana akiwa na viongozi mbalimbali nchini Kenya na nje ya Kenya.

image
na Radio Jambo

Habari26 November 2022 - 10:58

Muhtasari


  • Charlene Ruto amekuwa akifanya kazi kupita kiasi hivi majuzi huku wengi wakihoji hatua zake za hivi majuzi

Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino alitoa maoni na kumsifu bintiye Rais Ruto kwa kazi nzuri anayofanya.

Kwenye chapisho lililotolewa na Charlene Ruto leo ambapo aliomba kuambiwa jambo na wafuasi wake,Babu Owino alimwambia kwamba anaffanya kazi nzuri na siku moja atakuwa naibu wake.

Babu hakuweka wazi ni naibu wa nini au cheo kipi.

"Charlene Ruto unafanya kazi nzuri. siku moja utakuwa naibu wangu,"Babu Aliandika.

Charlene alijibu na kuthamini maoni hayo.

"ASante Babu Owino."

Charlene Ruto amekuwa akifanya kazi kupita kiasi hivi majuzi huku wengi wakihoji hatua zake za hivi majuzi.

Ameonekana akiwa na viongozi mbalimbali nchini Kenya na nje ya Kenya.

Alikuwa katika kaunti ya Narok leo na siku zilizopita alionekana Bomet, Kisii na Nairobi. Pia amekuwa akiwashirikisha vijana na kutembelea takriban kaunti zote nchini.

Mashabiki nao waliungana kumuunga mkono kwa kazi nzuri anayoifanya ingawa bado haijawekwa wazi nafasi anayoshikilia serikalini.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved