logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Cherargei ampongeza Linturi kwa kuweka mambo wazi huku akimsuta Kuria

Linturi alisema yeye ndiye msimamizi wa chakula kinahitajika kiasi gani na upungufu ni kiasi gani.

image
na Radio Jambo

Habari28 November 2022 - 13:51

Muhtasari


  • Katika taarifa yake Jumatatu, seneta huyo alisema serikali inafaa kutumia mahindi yanayopatikana humu nchini badala ya kuagiza kutoka nje
Seneta wa Nandi, Samson Cherargei

Seneta wa Nandi Samson Cherargei amepongeza hatua ya Waziri wa Kilimo Mithuka Linturi kufafanua kuwa Baraza la Mawaziri halikuhusika katika uagizaji wa mahindi.

Katika taarifa yake Jumatatu, seneta huyo alisema serikali inafaa kutumia mahindi yanayopatikana humu nchini badala ya kuagiza kutoka nje.

"Asante Waziri Mithika Linturi kwa kuweka rekodi kuwa baraza la mawaziri halikuidhinisha uagizaji wa magunia milioni 10 ya mahindi yasiyotozwa ushuru," alisema.

"Tumia mahindi yanayopatikana ndani ya nchi kuwahudumia wakulima Chochote ambacho CS kuria anavuta au kunywa Mungu anajua !!!. Mungu mbele !"

Hapo awali, Linturi alijitenga na maoni ya Waziri wa Biashara Moses Kuria kuhusu uingizaji wa mahindi.

Linturi alisema yeye ndiye msimamizi wa chakula kinahitajika kiasi gani na upungufu ni kiasi gani.

“Kwa hiyo sitajibu kinachoripotiwa kwenye mitandao ya kijamii,” alisema.

"Shika farasi wako maana nataka kukupa msimamo ambao niko tayari kuutetea. Nahitaji kuwa na takwimu kabla sijajibu hilo."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved