In Summary

• Kang'ethe alihukumiwa miaka 20 jela baada ya kupatikana na kosa la ubakaji.

Joseph Kang'ethe akikumbatiana na mamake mkongwe baada ya kurudi nyumbani akitoka jela alikokaa miaka 20
Image: JEPTUM CHESIYNA//THE STAR

Ilikuwa ni isiyo ya kawaida, siku ya furaha katika eneo bunge la Kuresoi Kaskazini, kijiji cha Mukinduri katika familia ya ajuza mmoja wa miaka 95 baada ya kijana wake kurejea kutoka jela alipohudumia kifungo cha miaka 20.

Joseph Kang’ethe mwenye umri wa miaka 69 sasa alihukumiwa miaka 20 iliyopita akiwa na miaka 49 katika gereza kuu la Nakuru.

Kang’ethe alipatikana na makossa ya ubakaji ambapo kifungo hicho kilimhusu.

Katika picha ambazo mpiga picha wetu alichukua, Kang’ethe na mama yake mkongwe walionekana wakikumbatiana kwa mapenzi ya mtoto kwa mama, huku ajuza huyo akipiga bismillah kwa kumuona tena mtoto wake ambaye walikuwa wametenganishwa naye kwa miongo miwili iliyopita.

Baada ya kuwasili nyumbani, Kang’ethe alipewa karibu kama shujaa kwani watu wengi walifurika nyumbani kwake kumuona kama kweli yuko mzima, kwani wengi walikuwa wanafikiri kama kioja kumuona mzee aliyehudumia kifungo cha miaka mingi na kurejea nyumani akiwa salama na aliyebadilika kimaadili.

- Joseph Kang'ethe akikumbatiana na mamake mkongwe baada ya kurudi nyumbani akitoka jela alikokaa miaka 20
- Joseph Kang'ethe akikumbatiana na mamake mkongwe baada ya kurudi nyumbani akitoka jela alikokaa miaka 20
- Joseph Kang'ethe akikumbatiana na mamake mkongwe baada ya kurudi nyumbani akitoka jela alikokaa miaka 20
- Joseph Kang'ethe akikumbatiana na mamake mkongwe baada ya kurudi nyumbani akitoka jela alikokaa miaka 20
- Joseph Kang'ethe akikumbatiana na mamake mkongwe baada ya kurudi nyumbani akitoka jela alikokaa miaka 20
- Joseph Kang'ethe akikumbatiana na mamake mkongwe baada ya kurudi nyumbani akitoka jela alikokaa miaka 20
View Comments