In Summary
  • Seneta Samson Cherargei amemtaka Matiangi kuwa jasiri na kuelewa kuwa alichowafanyia wengine ndicho kinachompata hivi leo
Aliyekuwa waziri wa usalama wa ndani Fred Matiang'i.

Seneta Samson Cherargei amedai kwamba aliyekuwa Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiangi anaonekana kuogopa sana katika Makao Makuu ya DCI ilhali ni dhahiri huo ndio mwanzo wa matatizo yake.

Kulingana na Cherargei, Matiangi atakabiliwa na madhara makubwa chini ya utawala wa Ruto na hilo halina shaka.

Fred Matiangi anajibu maswali katika Makao Makuu ya DCI kuhusu anachojua kuhusu uvamizi nyumbani kwake.

Ni dhahiri kuwa EACC pia imemwandikia barua mkuu wa utumishi wa umma kutaka kujua kiasi cha utajiri unaomilikiwa na Fred Matiangi.

Seneta Samson Cherargei amemtaka Matiangi kuwa jasiri na kuelewa kuwa alichowafanyia wengine ndicho kinachompata hivi leo.

"Matiangi anaonekana kuogopa kabla ya mchezo halisi kuanza. Alipokuwa CS mambo ya ndani alitumia kusisitiza kwamba polisi wako sahihi kila wakati licha ya maagizo kadhaa ya mahakama ikiwa ni pamoja na yangu ya Aprili 2022. alikuwa mkimbizi wa Haki.

Si akule maharagwe kidogo jamani kama mahubusu wengine."

Matiang'i alijiwasilisha katika makao makuu ya DCI siku ya Jumanne huku aiwa ameandamana na mawakili wake na baadhi ya wanasiasa wa mrengo wa Azimio.

 

 

 

 

 

View Comments