logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maneno yaliyotumiwa na adui dhidi yetu hayapaswi kuvumiliwa-Muhoozi

Muhoozi amekuwa kwenye vichwa vya habari kwa ajili ya maneno yake tatanishi kuhusu Afrika.

image
na Radio Jambo

Makala11 March 2023 - 07:08

Muhtasari


  • Aliendelea na kudai kuwa baadhi ya watu walikuwa wakitumia lugha ya matusi kama "Nigga" kumaanisha "Watu Weusi" ambayo haifai kuvumiliwa hata kidogo.
KWA HISANI

Mtoto wa Rais Yoweri Museveni ambaye ni Jenerali Muhoozi Kainerugaba amewasifu watu weusi akidai kuwa Waafrika ni watu wakuu.

Akitumia akaunti yake rasmi ya Twitter, Jenerali Muhoozi alidai kuwa ingawa Waafrika ni jamii kubwa zaidi duniani, kuna watu ambao walikuwa hawathamini hilo.

Aliendelea na kudai kuwa baadhi ya watu walikuwa wakitumia lugha ya matusi kama "Nigga" kumaanisha "Watu Weusi" ambayo haifai kuvumiliwa hata kidogo.

"Watu weusi wote ni wamaana! Sisi sote ni wazao wa watu wa kwanza! Kwa kweli, Waafrika ni jamii kubwa zaidi duniani! Maneno ambayo Adui aliyatumia dhidi yetu kama 'Nigga' HAYAPASI kuvumiliwa na sisi wenyewe! Lugha kama hiyo ni 'Marufuku'. ' kama tunavyosema kwa Kiswahili! Ni 'Haramu'." Jenerali Muhoozi Kainerugaba aliandika.

Muhoozi amekuwa kwenye vichwa vya habari kwa ajili ya maneno yake tatanishi kuhusu Afrika.

Jenerali huyo aligonga vichwa vya habari sana baada ya matamshi na madai yake ya kuteka nyara mji wa Nairobi.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved