In Summary
  • Viongozi hao walisema kuwa watafanya kazi na Serikali ya Kenya Kwanza kuhakikisha maendeleo katika mikoa ya Nyanza
ALIYEKUWA GAVANA WA NAIROBI EVANS KIDERO NA RAIS WILLIAM RUTO
Image: TWITTER

Viongozi wa Nyanza wakiwemo waliokuwa magavana Evans Kidero (Nairobi), Okoth Obado (Migori) na Jack Ranguma (Kisumu), wamethibitisha kujiunga na chama kinachoongozwa na Rais William Ruto United Democratic Alliance (UDA) 

Viongozi hao walisema kuwa watafanya kazi na Serikali ya Kenya Kwanza kuhakikisha maendeleo katika mikoa ya Nyanza.

Akizungumza wakati na waandishi wa habari katika makao makuu ya Chama cha UDA mnamo Jumanne, Machi 14, Kidero alisema kuwa chama tawala kinawajali watu wa Kenya na kuongeza kuwa muungano wa Azimio ulizingatia jambo lisilofaa.

Aidha, alisema kuwa hawatashiriki maandamano ya Azimio yanayoendelea na kuongeza kuwa yanawatenga Waluo Nyanza kutoka maeneo mengine ya nchi.

Tumesikia kuhusu maandamano na yatasababisha watu kuteseka. Tunaingia kwenye chama kinachojali watu wake na sio chama tulichoacha chenye nia ya machafuko.

"Chama kina nia ya kujifanyia mambo yao wenyewe na sio watu waliowachagua. Kulikuwa na maandamano Migori na mama zetu hawakuweza kuuza Omena kwa sababu shughuli za kawaida zililemazwa," Kidero alilalamika.

Zaidi ya hayo, Kidero alibainisha kuwa licha ya jamii ya Waluo Nyanza kutompigia kura Rais na Naibu Rais, wameweka eneo hilo kipaumbele linapokuja suala la maendeleo.

“Katika muda wa miezi mitatu, yeye (Rais) amewahakikishia watu wa Nyanza kwamba lazima tuwe sehemu ya Kenya. Tumeona ahadi ya Rais ya kujenga barabara mbalimbali za Siaya, Kisumu, Homabay na Migori,” akaongeza.

 

 

 

 

View Comments