logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamume amchoma kisu mke wake, kisha amuamsha binti yao kuona alichokifanya!

Alijaribu kujitoa uhai lakini majirani na polisi wakafika kwa wakati na kumzuia kujiua.

image
na Radio Jambo

Habari17 March 2023 - 04:40

Muhtasari


• Video iliyosambazwa kutokana na tukio hilo ilionyesha binti mdogo akilia sana huku akiliita jina la mama yake aliyefariki.

Kisu cha mauaji

Wakaazi wa Kasarani katika kaunti ya Nairobi walipigwa na butwaa baada ya mwanabodaboda mmoja eneo hilo kumuua mke wake usiku na kisha kumuamsha binti yake kuona kitendo alichomfanyia mama yake.

Kulingana na taarifa iliyopeperushwa na runinga ya Kameme, mwanamume huyo mhudumu wa Boda Boda alimuua mkewe kwa kumchoma kisu mara kadhaa kabla ya kujaribu pia kujitoa uhai lakini hakufanikiwa.

Jirani aliyezungumza na waandishi wa habari alisema muuaji huyo alimwamsha bintiye ambaye ndiyo kwanza amemaliza kidato cha nne na aliyekuwa sebuleni na kumwambia aende kuona kuwa amemuua mama yao.

“Akamwambia binti yake ‘amka uone nimemfanyia nini mama yako’ binti huyo alipomuona baba yake akiwa na kisu kikiwa kimepakwa damu alimsihi asimdhuru, akaenda chumbani na kumkuta mama yake tayari amekufa na kando yake kulikuwa na dadake mdogo na akamchukua," jirani huyo aliambia Kameme TV.

Mwanamume huyo alijaribu kujimaliza, lakini binti huyo jasiri alifaulu kutuma ujumbe kwa marafiki wa mama yake, ambao walizua hofu. Mwanamume huyo alikuwa amejaribu kujidhuru, lakini polisi walifika kwa wakati ili kumzuia. Pia waliuchukua mwili. Video iliyosambazwa kutokana na tukio hilo ilionyesha binti mdogo akilia sana huku akiliita jina la mama yake aliyefariki.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved