logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uhuru alikiendesha chama chake vibaya-Sossion

Akizungumza wakati wa mahojiano, alisema anachafua majina ya marais wastaafu.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri23 May 2023 - 08:44

Muhtasari


  • Katibu Mkuu huyo wa zamani wa KNUT aliendelea na kusema hatua za Uhuru zitaathiri utoaji wa huduma kwa utawala uliopo.

CAS wa Utalii Wilson Sossion Jumanne asubuhi alisema hatua za Rais wa zamani Uhuru Kenyatta ni aibu kwa eneo na kimataifa kwa ujumla.

Akizungumza wakati wa mahojiano, alisema anachafua majina ya marais wastaafu.

"Uhuru Kenyatta, kama rais wa zamani, anaweka utangulizi mbaya sana... Ukweli wa mambo unabakia kuwa Uhuru anakuwa aibu ya kikanda na kimataifa," alisema.

Alisema rais huyo mstaafu amekiendesha vibaya chama chake tawala.

"Ilifika wakati aliiacha serikali ya sasa ifanye kazi yake kwani muda wake ulikuwa umepita."

Katibu Mkuu huyo wa zamani wa KNUT aliendelea na kusema hatua za Uhuru zitaathiri utoaji wa huduma kwa utawala uliopo.

"Karibu yuko katika hatua ya kuvuruga utaratibu wa kisiasa wa nchi," alisema.

Sossion alikariri hisia za Waziri wa Ulinzi Aden Duale, ambaye mwishoni mwa juma alisema kwamba hatua za hivi majuzi za Rais huyo wa zamani zilikuwa za aibu.

Matamshi yake Sossion yanajiri siku moja baaa ya rais mstaafu Uhuru kuwafurusha wanachama 10 kutoka Jubilee, huku akiwateuwa viongozi wapya.

Kenyatta alisisitiza mnamo Jumatatu, Mei 22, 2023 kwamba hababaishwi na wanaotaka kumvua taji la uongozi chamani, akisema alivikwa kofia hiyo na wananchi.

Rais huyo wa tano wa Kenya alisema;

“Ningetaka wajue (wapinzani wake); Niliteuliwa na wananchi kuongoza chama, kisha wakanichague hadi nilipoachilia mamlaka na Wakenya ndio wataniondoa katika Jubilee.”

Alitoa matamshi hayo katika Kongamano la Kitaifa la Juibilee, mnamo Jumatatu, Mei 22, 2023 lililoandaliwa jijini Nairobi.

Majuzi, baadhi ya viongozi na wanasiasa wa Jubilee wanaoonekana kuegemea kwa serikali ya Kenya Kwanza walimbandua Kenyatta kutoka kwa wadhifa wake, nafasi yake ikitwaliwa na mbunge maalum Sabina Chege.

Katibu Mkuu wa chama hicho Bw Jeremiah Kioni, pia alivuliwa joho lake aliyekuwa mbunge wa Kieni Kanini Kega akitangazwa kumrithi.

Kenyatta na Kioni, hata hivyo, wakihutubu katika kongamano la Jubilee, walisisitiza kwamba wangali mamlakani.

Kwa upande wake rais huyo mstaafu, alionya wanaomchokoza akidai yeye hatishwi na yeyote.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved