In Summary

• Khalwale alikuwa akiitetea serikali ya kitaifa katika hotuba yake kwa waombolezaji Jumamosi wakati sehemu ilipoanza kumzonga.

• “Kama kiongozi mkuu zaidi Kakamega, sina budi kuwaambia watu wangu ukweli ili wajue taifa linaelekea wapi,” akasema huku kukiwa na manung’uniko.

Khalwale alikuwa akihutubia waombolezaji Kakamega alipoanza kutetea ushuru wa asilimia 3 kwa Wakenya ili kujengewa nyumba.
Image: Twitter

Seneta wa Kakamega Boni Khalwale alipata wakati mgumu kuhutubia waombolezaji kwenye ibada ya wafu baada ya baadhi yao kuanza kumzonga.

 

Khalwale alikuwa akiitetea serikali ya kitaifa katika hotuba yake kwa waombolezaji Jumamosi wakati sehemu ilipoanza kumzonga.

 

Seneta huyo alikuwa miongoni mwa viongozi wakuu waliohudhuria ibada ya mazishi ya mwanachama wa Maendeleo Democratic Party Joseph Amisi Omukanda-Shiyenga huko Navakholo, Kaunti ya Kakamega.

Amisi alikuwa kaka wa Katibu Mkuu wa Elimu ya Juu Beatrice Inyangala.

Seneta huyo alikasirika baada ya kujaribu kutetea Mswada wa Fedha 2023.

Khalwale alikuwa amewasuta baadhi ya viongozi waliozungumza mbele yake akisema walikuwa wakipotosha umati kuhusu suala la ushuru wakati hekaheka ilipoanza.

"Kuhusu suala la kodi, mnapaswa kujua kwamba yeyote anayewaambia kwamba ushuru umeongezwa anapotosha muswada wa bajeti utasomwa mwezi ujao. Huo ni ukweli," alisema.

Mara tu alipomaliza kusema, umati wa watu ulianza kupiga kelele za uwongo mara kwa mara.

“Uongo, unadanganya,” sauti ilisikika kutoka kwa umati huku wengine wakimwambia arudi kwenye kiti chake.

Deejay alilazimika kucheza muziki ili kuzuia heckling ambayo ilizidi.

Khalwale baadaye alimtaka Deejay kusitisha muziki na aliendelea na hotuba yake.

“Kama kiongozi mkuu zaidi Kakamega, sina budi kuwaambia watu wangu ukweli ili wajue taifa linaelekea wapi,” akasema huku kukiwa na manung’uniko.

Waombolezaji hawakukata tamaa.

Kelele za 'uongo' bado ziliendelea hata alipokuwa akisisitiza kuzihutubia.

"Ninakubali kwamba gharama ya maisha kwa sasa ni ya juu sana. Lakini kile ambacho viongozi wanapaswa kujadili ni jinsi watakavyofanya kazi ili kupunguza gharama za maisha," aliendelea hata wakati waombolezaji hao wakizidisha mbwembwe.

View Comments