logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mzee wa miaka 72 aanguka na kufariki saa chache baada ya kujiandikisha Inua Jamii

Hivi majuzi naibu rais Gachagua alifichua kwamba wameanzisha mpangpo wa kuwasajili wakongwe.

image
na Radio Jambo

Habari07 September 2023 - 07:02

Muhtasari


• Wakongwe hao walikuwa wamejitokeza asubuhi na walipanga foleni kwa muda mrefu kabla ya kusajiliwa.

Mzee mmoja wa umri wa miaka 72 katika eneo la Nyaribari Chache kaunti ya Kisii ameripitiwa kuanguka, kuzirai na baadae kuripotiwa kufariki dunia baada ya kumaliza kupanga foleni ya kusajiliwa katika mpango wa Inua Jamii ambao unashughulikia marupurupu kwa wazee wa Zaidi ya miaka 70.

Mzee huyo alisemekana kuzirai nje ya ukumbi wa jamii katika eneo la Keumbu ambapo mamia ya wazee wa Zaidi ya miaka 72 walikuwa wamepiga foleni ili kusajiliwa.

“Wakaazi wanailaumu serikali kwa mipango mbovu ambapo wazee kadhaa waliojitokeza tangu 6:00 asubuhi walikuwa wamesimama kwenye mlolongo kwa muda mrefu,” Chanzo kimoja cha habari kilisema.

Haya yanajiri ikiwa ni siku chache baada ya naibu rais Rigathi Gachagua kufichua kwamba tayari rais Ruto ametoa agizo la kusajiliwa upya kwa wazee wenye umri wa miaka 70 kwa mpango wa Inua Jamii kwa ajili ya kupokezwa shilingi elfu 2 kila mwezi.

“Rais ametuagiza tuanzishe tena kuandikisha wazee wa miaka 70 kwenda juu waanze kupata marupurupu yao,” Gachagua alisema wakati wa mkutano wa ugatuzi mjini Eldoret wiki chache zilizopita.

Katika hotuba yake, Naibu rais pia aliwaambia watu kwamba watamsajili kinara wa upinzani Raila Odinga katika mpango huo ili kumpokeza elfu 2 za kila mwezi katka njama ya kumsaafisha kutoka kwa siasa.

Na tukiandikisha hao nimemwambia PS huyu mzee wa kitendawili [Raila Odinga] umwandikishe akuwe anachukua elfu yake mbili kila mwezi ndio aende kupumzika,” Gachagua alisema huku watu wakimshangilia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved