logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uchumi ni mbaya: Mama mboga amdunga kisu puani ng'ombe aliyevizia biashara yake

Ng’ombe huyo anaonekana akitembea kando kando ya barabara akiwa na uchungu huku kisu hicho kikiwa bado kimekwama usoni

image
na Radio Jambo

Makala04 November 2023 - 05:55

Muhtasari


• Kwa mujibu wa toleo la Taifa Leo, kitendo hicho kilichohusishwa na hasira kutoka kwa mfanyibiashara huyo lilitokea majira ya jioni mnamo Oktoba 31.

Ng'ombe

Kisa cha kutatanisha kilishuhudiwa katika soko la Kitengela kaunti ya Kajiado baada ya mama mfanyibiashara mdogo wa mboga za majani kumdunga kisu puani ng’ombe aliyekuwa anazengua karibu na genge lake la mboga.

Kwa mujibu wa toleo la Taifa Leo, kitendo hicho kilichohusishwa na hasira kutoka kwa mfanyibiashara huyo lilitokea majira ya jioni mnamo Oktoba 31.

Kulingana na picha zilizopigwa na kusambazwa mitandaoni, ng’ombe huyo anaonekana akitembea kando kando ya barabara akiwa na uchungu huku kisu hicho kikiwa bado kimekwama usoni karibu na pua lake.

Huku baadhi ya wakazi wakitaka shirika la ulinzi na matunzo kwa wanyama (KSPCA) kufuatilia tukio hilo na kumwokoa ng’ombe huyo, baadhi walitaka mwanamke huyo atiwe mbaroni mara moja kwa kitendo hicho cha kikatili, Taifa Leo walieleza.

Wengi wanakisia kwamba huenda mwanamke huyo alitenda kitendo hicho kwa kukerwa na mifugo ambao mara nyingi huonekana wakizurura katika maeneo ya masoko pasi na wenyewe.

Mama Mboga alitekeleza ukatili huo pasi na kupenda kwani uchumi umekuwa mbaya kiasi kwamba watu wamepatwa na msongo wa mawazo wengine hadi kufikia hatua za kufanya mambo kama hayo pasi na kupenda kwao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved