In Summary
  • Sudi alisema kuwa Miguna na viongozi wengine walikuwa wamejipenyeza katika harakati nzuri ya uwajibikaji ambayo ilikuwa imeanzishwa na Gen Z.
Mbunge wa Kapseret Oscar Sudi
Image: MAKTABA

Mbunge wa Kapseret Oscar Sudi mnamo Jumatatu, Julai 29, alimsuta Miguna Miguna akimshutumu kwa kuchochea vijana wa Kenya kuasi serikali.

Sudi alisema kuwa Miguna na viongozi wengine walikuwa wamejipenyeza katika harakati nzuri ya uwajibikaji ambayo ilikuwa imeanzishwa na Gen Z.

Mbunge huyo aliendelea kudai kuwa yeye ndiye alimwambia Rais William Ruto amondoe Miguna ili arejee Kenya baada ya kufurushwa na aliyekuwa Rais wa Kenya Uhuru.

"Nilishangaa kwamba mtu mzee kama wewe angeweza kuchochea Gen Z ambao ni watoto wetu," Sudi alifoka.

Alieleza kuwa uchochezi huo mara nyingi ulitokea kwenye X Spaces ambapo Miguna ni mshiriki.

"Gen Z walipoanza maandamano yao, niliwaunga mkono kwa sababu walikuwa na maswala ya kweli. Nilijua sasa walikuwa wamekomaa na kuelewa masuala ya utawala,” Sudi alieleza.

Kulingana na Sudi, lengo kuu la Miguna na viongozi wengine wanaoshangilia maandamano ni kuona Kenya ikiangukia kwenye uasi na vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Alishangaa kwa nini Miguna alishangilia kukaliwa kwa Bunge na afisi zingine za kikatiba.

"Tuangazie masuala yetu kwa njia ambayo hatutaharibu nchi," aliwahimiza Wakenya.

Akizungumzia wakati wa Miguna uhamishoni, Sudi alisema kwamba alijutia kurudi kwa Miguna miaka mitatu baada ya Miguna kurejea nchini 2022.

Kulingana na Sudi, alimkaribisha Miguna mara tu alipowasili nchini Kenya lakini baada ya mazungumzo ya saa 3 akagundua ni kwa nini utawala wa zamani ulimfukuza.

 

 

 

 

 

View Comments