Bunge la kaunti lafungwa
Bunge la kaunti ya Kericho lafungwa baada ya mfanyikazi mmoja kupatikana na corona
wafanyikazi washauriwa kuchukua likizo
- Afisi za gavana na naibu wake kufungwa pia
Bunge la kaunti ya Kericho limesitisha oparesheni zake kwa siku 15 baada ya mfanyikazi mmoja kupatikana na virusi vya corona .
Katika arifa iliyotumwa na karani wa bunge hilo Martin Epus amewashauri wafanyikazi wote wa bunge hilo kuchukua likizo kuanzia ijumaa tarehe 23 oktoba .
Hakutoa maelezo kuhusu kisa hicho lakini badala yake alisema habari hizo zimekuwa zikisambaa katika mitandao ya kijamii .
Karani huyo amesema ni wafanyikazi wachache pekee wanaotoa huduma za kimsingi kama vile usalama , Uhasibu na huduma za kamati ndio watakaoruhusiwa bungeni .
Epus aliongeza kwamba mpango umewekwa ili kuwapima wafanyikazi wote wa bunge hilo .
Wakati huo huo karani huyo amewashauri wafanyikazi wa kaunti kufuata kanuni zote zilizotolewa na wizara ya afya kuzuia kusambaa kwa virusi vya corona
Bunge la kaunti ya Kericho linajiunga na lile la Homabay ambalo lilifungwa kwa wiki mbili baada ya mwakilishi mmoja wa kaunti kupatikana na virusi vya kaunti .
Bunge la kaunti ya Nandi pia lilisitisha oparesheni zake kwa muda katika makao yake makuu ya Kapsabet baada ya maafisa wanane wakuu kupatikana na Corona .
Katibu wa kaunti Francis Sang amesema jumatatu kwamba maafisa hao wanane kutoka idara za afya,Fedha ,elimu na mipango ya kiuchumi .Alisema idara zilioathiriwa pamoja na afisi za gavana na naibu wake zitafungwa kwa siku 14.