Shambulizi
Kinyozi ashtakiwa kwa kumkata mwenzake kidevuni
Makori alichukua kisu na kukitumia kumjeruhi kidevuni
- Kesi hiyo itatajwa Novemba tarehe 11.
- Aliketi nje ya eneo hilo la kunya akimngoja mmiliki wa biashara hiyo kuwasili
Kinyozi mmoja ameshtakiwa kwa kumjeruhi mwenzake kutumia kisu kwa kumkata kidevuni .
Silus Makori alishtakiwa katika mahakama ya kibera baada ya kufikishwa mbele ya hakimu mkuu Philip Mutua ambapo alikanusha mashtaka dhidi yake
Kulingana na uchunguzi wa polisi Philip Otieno aliwasili mahali pake pa kazi ambapo alikutana na Makori na kuitisha ampe mashine ya kunyolea lakini mtuhumiwa alimpuuza .
Kisha aliketi nje ya eneo hilo la kunya akimngoja mmiliki wa biashara hiyo kuwasili .Ni wakati huo ambapo Makori alichukua kisu na kukitumia kumjeruhi kidevuni .
Rafiki zake walikimbia kumsaidia na kumpeleka hospitalini ambapo aliibiwa na baadaye akaripoti tukio hilo kwa polisi .Makori aliachiliwa kwa bondi ya shilingi elfu 30 na mdhamini wa kiasi kama Hicho .Kesi hiyo itatajwa Novemba tarehe 11.