Mfute Kinoti kazi!
Kihika amtaka Uhuru kumfuta kazi Kinoti kuhusu kesi za PEV
washirika wa Ruto wamzidishi Kinoti shinikizo
- Wiki jana palikuwa na ripoti kwamba Kinoti anapanga kuzifufua kesi za ghasia za baada ya uchaguzi
- Washirika wa Naibu wa rais wamelaani sana hatua hiyo huku rais kenyatta pia akimshtumu Kinoti kwa mpango huo
Mkurugnzi wa DCI George Kinoti ameendelea kujipata chini ya shinikizo kufuatia matamshi yake ya hivi maajuzi kuhusu kesi za baada ya uchaguzi wa mwaka wa 2007/2008 .
Washirika wa naibu wa rais William Ruto sasa wanamtaka rais Uhuru Kenyatta kumfuta kazi Kinoti kuhusu matamshi yake .wabunge hao wakiongozwa na seneta wa Nakuru Susan Kihika walikuwa wakatika mazishi ya mamake mbunge wa Bahati Kimani Ngunjiri Edith Ngunjiri . mbunge wa mathira Rigathi Gachagua alikariri matamshi ya rais kwamba maafisa wa serikai wanafaa kufikiria kwanza kabla ya kuchukua hatua kama hizo .Amesema taifa limeshapga hatua mbele na matamshi ya Kinoti yalitishia Amani katika eneo la Rift Valley .
Gachagua amesema Kinoti hafahamu jinsi rais na naibu wake walivyofaulu kuleta Amani katika eneo la Rift valley .
“ Una kazi nyingi za kufanya . anza na watu waliopora pesa za covid 19 kabla ya kuvuruga Amani iliyopo sasa’ Gachagua amefoka
Seneta wa Nakuru Susan Kihika naye amemshauri rais Uhuru Kenyatta kumfuta kazi Kinoti akisema kwamba amekosa maadili kuhusu anavyoshughulikia suala hilo la ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka wa 2007/2008 .
“ Kinoti anafaa kuwa amefutwa kazi au angekuwa na ustaarabu angekuwa ameshajiuzulu . mtu kama huyo ambaye hana hadhi hafai kuongoza idara ya uchunguzi nchini ‘ Kihika amesema . seneta huyo amesema Kinoti ni mtu ambaye anaweza kumbandikia mtu madai na kuweka ushahidi dhidi ya mtu asiye na hatia
Kihika ameongeza kwamba Amani ya sasa nchini haifai kutishiwa na watu walio na hila .