In Summary

 

  •  Amesema wafanyikazi wanaokubali kutumiwa na wanasiasa wanatishia kulirejesha taifa katika kipindi kibaya cha ukabila .
  •  Ruto amewaambia wafanyikazi wa umma walio na jukumu la kuwalinda wananchi kutotumia nafasi zao kufanya mabaya  kwani hatua hiyo itakuwa hatari kwa nchi .

 

Naibu wa Rais William Ruto

 Naibu wa rais William Ruto  amewaonya wafanyikazi wa umma dhidi ya kutumiwa vibaya na wanasiasa  kwa kukiuka sheria kupitia utumizi mbaya wa maamlaka na afisi zao .

 Akizungumza huko Nakuru  wakati wa mazishi ya mamake mbunge wa  Bahati Kimani Ngunjiri ,Ruto amesema  wanaolenga kuvuruga  mshikimano wa kijamii uliopo sasa wana hila .

 Amesema wafanyikazi wanaokubali kutumiwa na wanasiasa wanatishia kulirejesha taifa katika kipindi kibaya cha ukabila .

 

“ Badala ya  kukabiliana na uhalifu ulipo sasa nchini ,wanataka kuwachochea  wananchi  kuendeleza ukabila’ amesema Ruto .

 Aliongeza kusema ‘ Nataka kuongeza kwamba kutumia mfumo wa idara za uchunguzi na mashtaka kuwakandamiza watu wa kabila Fulani  au mrengo fulani wa kisiasa ni jambo baya’

 Amesema kuna watu walionufaika pakubwa na siasa za uhasama  na ukabila  na  wamegundua kwamba hawana manufaa ya kupata wakati pana amani nchini .

 “ Wanajaribu kuwatumia watumishi wa umma kuvuruga Amani miongoni mwa wakaazi wa Rift Valley … wafanyikazi wa umma wamecha kazi zao na sasa wanapiga siasa ..wanafanya kazi ya  shetani  na nataka kuwaambia kwamba hawatafaulu ..’

 Ruto amewaambia wafanyikazi wa umma walio na jukumu la kuwalinda wananchi kutotumia nafasi zao kufanya mabaya  kwani hatua hiyo itakuwa hatari kwa nchi .

  

View Comments