Tutangoja
Kenya huenda ikangoja chanjo ya Covid 19 hadi mwezi machi huku India ikipiga marufuku uagizaji wa chanjo hiyo
Poonawalla hata hivyo amesema uagizaji wa chanjo ya Co vax huenda usianze hadi machui au Aprili kwa sababu ya agizo la serikali ya India
- Kenya ilitarajia kupata chanjo ya Oxford -AstraZeneca mwezi ujao kutoka kwa kampuni ya Serum Institute of India (SII).
- Hata hivyo afisa mkuu mtendaji wa SII Adar Poonawalla siku ya jumapili amesema kampuni yake imezuiwa kutoa chanjo hiyo nchini India ahadi itoe dozi milioni 100 kwa serikali ya India.
Kenya italazimika kungoja kwa muda zaidi kwa chanjo ya corona abaada ya India kupiga marufuku kutolewa kwa chanjo hiyo kutoka nchini humo hadi mataifa mengine kwa miezi kadhaa ili kuwachanja watu walio katika hatari ya kuambukizwa .
Kenya ilitarajia kupata chanjo ya Oxford -AstraZeneca mwezi ujao kutoka kwa kampuni ya Serum Institute of India (SII).
Hata hivyo afisa mkuu mtendaji wa SII Adar Poonawalla siku ya jumapili amesema kampuni yake imezuiwa kutoa chanjo hiyo nchini India ahadi itoe dozi milioni 100 kwa serikali ya India.
“ Tunaweza tu kuipa serikali ya India chanjo wakati huu’ amesema Poonawalla katika mahojiano akiongeza kwamba anaunga mkono uamuzi huo .
Kenya mwezi Disemba ilituma ombi kupitia Covax ili kupewa dozi milioni 24 za chanjo hiyo na ilitarajia kupewa dozi milioni 12 za mwanzo mwishoni mwa mwezi huu au mapema mwezi februari .
“ Tumeagiza chanjo . tunataraji kwamba chanjo hiyo itakuwa hapa kufikia mwisho wa januari ama mwezi wa Februari’ alisema waziri wa Afya Mutahi Kagwe siku ya Ijumaa .
Poonawalla hata hivyo amesema uagizaji wa chanjo ya Co vax huenda usianze hadi machui au Aprili kwa sababu ya agizo la serikali ya India
Chanjo ya AstraZeneca ilipewa idhini ya dharura na serikali ya India siku ya jumapili lakini kwa masharti kwamba SII isiuze chanjo hiyo kwa nchi nyingine hadi watu walio katika hatari ya kuambukizwa virusi vya Corona wachanjwe nchini India .